Asha Bilal
Na Andrew Chale
“LEO
ndio Leo, lile Onesho la Usiku wa Khanga za Kale 2013, ‘Extra Vaa Khanga
Party’ ndani ya Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo Ijumaa ya
Novemba 8.
Katika
onesho hilo, jioni ya leo, Mke wa wa Makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Bi Asha Bilal anatarajia kuwa mgeni rasmi katika
kusindikiza usiku huo ambao pia utapambwa na mastaa mbalimbali wa ndani
na nje ya nchi, ikiwemo burudani murua kutoka kwa bendi ya Mashauzi
Classic.
Mkurugenzi
wa Fabak Fashion, Asia Idarous, ambao ndio waandaji wa maonyesho hayo,
amesema tofauti na maonyesho mengine yaliyotangulia, Kanga ya Kale ya
mwaka huu ina ladha tofauti kidogo ilikuwapa radha wadau wake..
“Licha
ya kuonyesha matoleo mapya na mitindo ya kanga pia kuonyesha yale ya
zamani ili kuleta vionjo zaidi kwa wavaaji wa sasa, tunakusudia kutoa
darasa kuhusiana na thamani ya kanga japo kwa muda mfupi tu”, alisema.
Na
kuongeza kuwa, usiku huo vazi la khanga ndilo litakuwa maalumu kwa wadau
watakaohudhuria sambamba na kupinga matumizi ya dawa za kulevya.
Kiingilio
katika onyesho hilo ni sh 30,000 na viti maalumu itakuwa ni sh 50,000
ambako tiketi zinaendelea kuuzwa Fabak Fashions Mikocheni na Gift Shop
Serena Hotel pamoja na mlangoni hapo hapo Serena hotel.
Aidha,
usiku wa Khanga za Kale umedhaminiwa na Redd’s, CXC, Clouds FM, Vayle
Spring, Magic FM, Eye View, Amina Design, Kabile, Voice of America,
Origin Unite, Channel Ten, DTV, Times FM, Michuzi Media Group, Event
Light na Miss Tanzania, New Africatv.com, Kajuna blog,Vijimambo blog na
wengineo kibao.
Maonyesho ya Kanga za kale nchini yanafanyika kwa mara ya tano tangu pale yalipoanzishwa rasmi mwake mwaka 2008


0 comments:
Post a Comment