ads

Habari Mpya

Monday, December 30, 2013

Radi yauwa watu nane Malawi

Soko mjini Lilongwe, Malawi
Watu wanane wamekufa nchini Malawi wakati radi ilipopiga kanisa katika mji mkuu, Lilongwe.
Walioshuhudia wanasema kulitokea mtafaruku katika kanisa la Sabato baada ya jengo la kanisa kupigwa na radi Jumamosi jioni.
Wakuu wa afya wanasema mtoto mmoja ni kati ya watu waliokufa.
Wameeleza kuwa watu 40 wengine wanatibiwa katika hospitali kuu.
Vyombo vya habari vya Malawi vinaripoti kuwa radi iliuwa watu watatu wengine katika matukio mbali-mbali tangu majira ya mvua kuanza mwezi uliopita.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: Radi yauwa watu nane Malawi Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top