ads

Habari Mpya

Thursday, February 20, 2014

JINSI YA KUJIWEKEA MAZINGIRA BORA YA MAFANIKIO BINAFSI KIMAISHA


Jifunze kuwa na kuongozwa na malengo.
Mara nyingi tumejikuta tukiwa kwenye mijadala na tukilalamikia umasikini wetu kusababishwa na wazungu, nyimbo hizi zimeanza miaka mingi na kwa kadri tunavyozidi kulalama ndivyo jinsi umasikini unavyo tuzidi siku baada ya siku. Tuna pumbazika  tulilaani mabara ya ulaya na marekani kwa kusababisha umasikini wetu wakati asilimia kubwa ya watu wa mabara hayo wapo hapa kwetu miaka hii na wanazidi kufanikiwa kwa kutumia vilivyopo hapahapa na isi tukiwa hapahapa tukiwatolea macho. Mtazamo wangu niwatofauti kidogo, na ninaungana na baadhi ya tafiti ambazo zimebainisha kuwa tatizo letu kubwa limekuwa sio sana mtaji, ardhi au elimu bali ni Matumizi mabaya ya muda, na Maisha yasiyokuwa na malengo.

Msingi wa malengo yetu uwe kwenye kuwekeza katika ufanisi na kuweka kipaumbele kwenye mafanikio yetu binafsi. Mipango mingi ya watu, hususan watu wa dunia ya tatu imekuwa isiyohalisi na isiyoishia kwenye mafanikio maana haikuhusishwa na muda muafaka , wenzetu wana msemo usemao“ No plan without Time span” yaani hakuna mpango au lengo lisilo endana na muda.

Malengo yamegawanyika katika makundi mawili, Malengo ya muda mrefu “Long term goals” na malengo ya muda mfupi “short term goals”. Malengo ya muda mrefu ni ilemipango ambayo inatuchukua muda mrefu kuitekeleza, kamavile ujenzi, elimu binafsi au ya watoto, kutafuta mwenza wa maisha nk. Malengo ya muda mfupi ni ile mipango ambayo tunaweza kuitekeleza kwa muda mfupi, kamavile kununua mavazi, kufanya usafi, kuandaa sherehe  nk. Mara nyingi inasemekana kwamba malengo ya muda mrefu yanaweza kufikiwa kiufanisi ikiwa yale ya muda mfupi yamekamilishwa vema. 

Katika kuweka malengo marazote jaribu  kufikiria yafuatayo;
1. Nini ninachotarajia kukifikia au kukipata katika lengo hili? “end product of your goal”, usijiwekee lengo tu bila kupata picha ya matokeo. Picha ya matokeo yanayoletwa na lengo hilo inamchango mkubwa sana katika kuchochea au kudumaza  ari yako kwenye kulifikia lengo husika.

2Ni mikakati na rasilimali gani itakayo tumika katika kulifikia lengo husika. Wengi hukaa kwenye vikao wakipanga mipango mingi ya kuanzisha miradi fulani bila kuwaza juu ya mikakati na rasilimali zitakazotumika na mara tu wanapoanza kutekeleza mipango yao hukutana na ugumu na ghafla husitisha mradi au kuuahirisha kabisa. Wewe ni shahidi wa nyumba nyingi zilizoanzwa na kusitishwa, Biashara nyingi zimefunguliwa kwa nguvu ya soda na ghafla kufungwa, watoto wengi wamejikuta wakipelekwa shule Fulani walizoziona ni nzuri na gharama na ghafla hawakumaliza mwaka wakahamishwa kukimbilia unafuu. Haya yote ni mazingira ya watu wanaojaribu kuweka malengo pasipo kuangalia mikakati au rasilimali zitakazo hitajika.

3Niwatu gani ambao nitawahitaji katika kulifikia lengo. Ni vizuri kujua kuwa kamwe hatuwezi kufikia malengo yetu kwa kutegemea jitihada zetu wenyewe, iko sehemu ambayo lazima utamwitaji mwingine. Wako waliojaribu kuanza mipango yao Fulani wakidhani hawatamhitaji binadamu yeyote, mara uhitaji ukatokea na kukawa na ulazima wa baadhi ya watu kuhusishwa, hapo ugumu mkubwa ukaanza. Ni vema kuishi na watu vizuri maana hujui wapi utamhitaji nani kwa kusudi gani. Wako pia walioshindwa kufikia malengo yao maana walifanya uchaguzi mbaya wa nani wa kumhusisha malengo yao. Sio kila mtu ni mtu sahihi kuhusika katika lengo lako, wako ambao unaweza kuwaambia tu waelewe nini kinaendelea na sio kushiriki, na pia wapo ambao waweza kuwahusisha katika mchakato mzima. Ugumu unakuwa kwenye hekima ya kuweza kutambua nani aelezwe pasipo kushiriki na nani aelezwe na kushiriki. Unaweza ukafanya uchaguzi mbaya na ukawa na lengo zuri kabisa lakini waliohusishwa wakaua lengo lako au kulitaifisha.
Itaendelea..........
IMEANDALIWA NA CHRISS MAUKI
MTAALAM WA SAIKOLOJIA NA JAMII (UDSM)
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: JINSI YA KUJIWEKEA MAZINGIRA BORA YA MAFANIKIO BINAFSI KIMAISHA Description: Rating: 5 Reviewed By: Unknown
Scroll to Top