Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kwamba Mjumbe wa Tume ya
Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengodo Mvungi(Pichani) amefariki katika
hospitali ya MillPark huko Afrika ya kusini alikokuwa akipata matibabu.
Dk Mvungi alijeruhiwa kwa kukatwa na mapanga kichwani Novemba 13, mwaka
huu nyumbani kwake Kibamba Msakuzi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam
na kulazwa Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (Moi) na baadaye kuhamishiwa
Hospitali ya Milpark, Johannesbarg, Afrika Kusini. : Kwa mujibu wa
Hussein Bashe Bashe “Dr Sengondo Mvungi Is No More,Taarifa zilizonifikia
kutoka Milpark Hospital Ndg yetu Mvungi Amefariki,Mnamo Majira ya Saa
Tisa na Nusu.Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi.
Wahalifu wamekatisha Uhai wake wakati akifanya Jukumu zito kwa Ajili ya
Taifa letu.Jambo hili linaumiza sana Mungu Atalipia Uhalifu huu. poleni
Tume ya Katiba,Poleni Familia,Poleni NCCR.
0 comments:
Post a Comment